WAKANDARASI WATAKIWA KUNUNUA VIFAA VINAVYOTENGENEZWA NCHINI.


Waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi mikubwa kununua vitendea kazi vinavyozalishwa hapa nchini ikiwemo mabomba ya kusafirisha maji kwa lengo la kukuza uchumi wa ndani.


Image result for PICHA YA ISACK KAMWELWE WAZIRI WA MAJI
Waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi Isack

Mh Kamwelwe ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wafanyakazi wa mamlaka ya maji safi na maji taka mkoa wa Dar-es-salaam na Pwani DAWASA,ambapo ameutaka uongozi wa DAWASA kulisimamia agizo hilo kwa umakini mkubwa .


Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa DAWASA Romanus Mwandingo amesema kuwa taratibu za ujenzi wa miradi mipya ya maji taka na maji safi likiwemo bwawa la kidunda linaendelea vizuri.

Hata hivyo agizo hilo la Mh waziri limekuja siku chache baada ya rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli kuagiza kutumika kwa bidhaa zinazozalishwa hapa nchini katika mkutano wa 11 wa wafanyabiashara kuliko kuagiza bidhaa za nje hali inayosababisha viwanda vya ndani kufa.

WAKANDARASI WATAKIWA KUNUNUA VIFAA VINAVYOTENGENEZWA NCHINI. WAKANDARASI WATAKIWA KUNUNUA VIFAA VINAVYOTENGENEZWA NCHINI. Reviewed by safina radio on March 21, 2018 Rating: 5

No comments