IMEELEZWA KUWA BANDARI YA MTWARA INAKUWA KWA KASI.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya
Udhibiti Maji na Nishati Zanzibar ZURA Mwalimu Ally Mwalimu, amesema kuwa Bandari
ya Mtwara inakuwa kwa kasi na bado ina fursa za uwekezaji .
SEHEMU YA BANDARI YA MTWARA |
Mwenyekiti huyo amesema hayo mara baada ya
kutembelea bandari hiyo kwa ajili ya kuangalia na kujifunza mambo mbali mbali na
kuweza kuona namna watakavyoweza kutumia bandari hiyo kusafirisha mafuta na
bidhaa nyingine.
Aidha, Bw. Mwalimu amesema kuwa Zanzibar wanataka
kutafuta njia rahisi za kusafirisha
mafuta kutoka bandari za Tanzania ambapo
awali walikuwa wakichukua mafuta kutoka bandari ya Dar es salaam lakini kutokana
na changamoto za bandari hiyo wameamua kupeleka katika bandari nyingine ikiwemo
ya Mtwara.
Kwa upande wake Mratibu wa Sekta ya Maji kutoka
ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kosmasi Komba amesema kuwa ni jambo la kujivunia
kuwa shughuli zinazofanywa na bandari
hiyo kuwa zinagusa watu na kwenda kujifunza.
Hata hivyo,
Bandari ya Mtwara inauwezo wa kusafirisha tani laki nne za mizigo mbali mbali
kwa mwaka ambapo hadi kumalizika kwa ujenzi wa Gati mpya mwezi Aprili mwaka 2019 itakuwa na uwezo wa
kusafirisha tani laki sita kwa mwaka.
IMEELEZWA KUWA BANDARI YA MTWARA INAKUWA KWA KASI.
Reviewed by safina radio
on
March 27, 2018
Rating:
No comments