Imebainika kuwa viapo vya miungu vinavyotoka kwenye madhabahu za koo na familia ni kisababisho kikubwa kinachowafanya vijana kukosa ajira
Imebainika
kuwa viapo vya miungu vinavyotoka kwenye madhabahu za koo na familia ni
kisababisho kikubwa kinachowafanya vijana kukosa ajira,kutokuolewa au kuoa kwa
wakati na wengine kujiingiza kwenye matendo maovu yakiwemo
matumizi ya dawa za kulevya.
Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi wa maombi
ulioko Mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili hadi saa sita mchana imekuandalia
maombi maalum ya kuvunja viapo vya miungu vinavyotoka kwenye koo na familia ili
kukomboa fursa za vijana kwa kukanyaga mafuta kama kitendo cha imani.
Aidha kwa mujibu wa somo hilo viapo vya miungu
vinavyotoka kwenye madhabahu vimewafanya vijana wengi kukwama kimaisha hasa
kwenye mahusiano,ajira,pamoja na elimu jambo ambalo kanisa jamii na taifa kwa
ujumla hawana budi kwenda mbele za Mungu
kwa maombi ili kuvunja viapo hivyo.
Pamoja na hayo maombi yatafanyika kwa vijana wote
ili kuwafungua dhidi ya roho ya mauti,magonjwa,mahusiano kuvunjika,ukosefu wa
ajira, kukomboa vibali vya karama na vipawa, pamoja na makundi yanayoshikiliwa
kwenye vifungo vya ulevi,zinaa na matumizi ya madawa ya kulevya.
Hata hivyo maombi hayo yanayokwenda sambamba na
kitendo cha imani cha kukanyaga mafuta yamelenga kufungua fursa mbalimbali za
vijana ili wawekwe huru na kutumikia kusudi la Mungu lililowekwa ndani mwao.
Imebainika kuwa viapo vya miungu vinavyotoka kwenye madhabahu za koo na familia ni kisababisho kikubwa kinachowafanya vijana kukosa ajira
Reviewed by safina radio
on
March 21, 2018
Rating:
No comments