HUDUMA YA REDIO SAFINA KESHO KATIKA UKUMBI WA MAOMBI, IMEANDAA MAOMBI MAALUMU YA KUSHUGHULIKIA ROHO YA UTUMWA INAYOWASABABISHIA WATU KUINGIA KATIKA WIMBI LA MADENI KWENYE JAMII.
ARUSHA.
Imebainishwa kuwa kuna uwezekano mkubwa wa adui
kuachilia roho ya madeni kwa watu endapo hawatasimama kikamilifu kumshirikisha
Mungu kila jambo wanalolifanya hususan biashara.
Kuingia katika wimbi la madeni kutokana na roho ya madeni inayoachiliwa na adui. |
Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi wa maombi
uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana
imekuandalia maombi maalumu ya kushughulikia roho ya utumwa inayo wasababisha
watu kuingia katika wimbi la madeni kwenye jamii.
Aidha kwa mujibu wa somo hilo roho ya madeni imekuwa
ikiwatesa baadhi ya watu Kutokana na kushidwa kulipa madeni hayo kwa wakati
hali ambayo imevuruga ndoa pamoja na watu kufisiliwa vitu vyao kama vile
nyumba,vyombo vya ndani,mifugo,mashamba pamoja na bidhaa walizonunua hata kama
hazitokani na fedha walizokopa.
Vilevile somo hilo limebainisha kuwa licha ya roho
ya madeni kusababisha watu kufisiliwa pia imesababisha magonjwa kama vile
ugonjwa wa moyo ,kisukari,shinikizo la damu na mara nyingine watu kupoteza
maisha kutokana na mshtuko pamoja na msongo wa mawazo.
Hata hivyo kesho watu wataombewa kulingana na
mahitaji yao hivyo kila mmoja anashauriwa kuwa na imani pamoja na kujipatanisha
na Mungu kwa njia ya maombi ya toba ili Mungu awaze kuwaokoa dhidi ya matatizo
hayo yanayowakabili.
HUDUMA YA REDIO SAFINA KESHO KATIKA UKUMBI WA MAOMBI, IMEANDAA MAOMBI MAALUMU YA KUSHUGHULIKIA ROHO YA UTUMWA INAYOWASABABISHIA WATU KUINGIA KATIKA WIMBI LA MADENI KWENYE JAMII.
Reviewed by safina radio
on
March 14, 2018
Rating:
No comments