WAZIRI JAFFO ASEMA LENGO LA RAIS KUANZISHA VIWANDA LIMEFIKIA ASILIMIA 49
Waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na
serikali za mitaa Mh Suleman Jaffo amesema kuwa lengo la rais la kuanzisha
viwanda mia moja kwa kila mkoa limefikia asilimia 49 katika kipindi cha miezi mine
tangu agizo litolewe na rais John Magufuli.
WAZIRI SULEMAN JAFFO |
Mh Jaffo amesema hayo mjini Dodoma katika kikao
kilichowahusisha wakuu wa mikoa makatibu tawala na watendaji waandamizi mikoa kwa
ajili ya kuandaa bajeti itakayowasilishwa bungeni wakati wa bunge la bajeti.
Amesema kuwa uanzishwaji wa viwanda hivyo mia moja
ulikuwa haujawahi kufanywa na wakuu wa mikoa yeyote katika historia ya nchi hii
hivyo wakuu hao wa mikoa watakuwa wa kwanza kuanzisha viwanda hivyo.
Kwa upande wake naibu katibu mkuu TAMISEMI Dr
Zainabu Chaula amesema kuwa utekelezwaji wa maagizo ya serikali utafanikiwa
endapo viongozi wa mikoa wataenda pamoja katika utendaji kazi.
Naye mwenyekiti wa wakuu wa mikoa hapa nchini
Mhandisi Evarest Ndikilo ameomba kufanyika kwa mkutano wa pamoja kati ya wakuu
hao wa mikoa na watendaji wa taasisi zinazosimamia masuala ya viwanda.
WAZIRI JAFFO ASEMA LENGO LA RAIS KUANZISHA VIWANDA LIMEFIKIA ASILIMIA 49
Reviewed by safina radio
on
March 21, 2018
Rating:
No comments