SIDO MANYARA, YAKUTA NA WAJASIRIAMALI WA VIWANDA VIDOGO VYA KUSINDIKA VYAKULA.
Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Nchini (SIDO)
Mkoani
Manyara limekutana na Wajasiriamali wa viwanda
vidogo vya kusindika vyakula Mkoani humo kwa lengo la kuwafundisha namna
bora ya kupata mikopo katika benki ya CRDB kupitia skimu ya SIDO.
Meneja wa SIDO Mkoani Manyara Abel Mapunda amesema
kuwa shughuli za sido ni kuendeleza teknolojia kwa
wajasiriamali, kutoa elimu ya ujasiriamali, biashara na masoko pamoja na
kuwapatia wajasiriamali mikopo ili waweze kujienedeleza kiuchumi.
Aidha, amesema kuwa SIDO imeingia mkataba na watu wa Benki ya CRDB
chini ya skimu ya SIDO ili kuwawezesha wajasiriamali hao kupata mikopo
mikubwa ambayo itawawewzesha kuendesha viwanda vyao pamoja na kujiinua
kiuchumi.
Naye Meneja Biashara kitengo cha mikopo CRDB Denis
Kashasha amesema kuwa wana makubaliano kati yao na SIDO kwaajili ya
kuwakopesha wajasiriamali wadogo lakini mpaka sasa hakuna mjasiriamali
aliyeweza kupata mkopo huo kutokana na kushindwa kutimiza vigezo.
Kwa upande wao wajasiriamali wamelalamikia masharti magumu
yaliyowekwa na benki ya CRDB kupitia Mkopo wa skimu ya SIDO na kuwasababishia
kushindwa kupata mikopo.
SIDO MANYARA, YAKUTA NA WAJASIRIAMALI WA VIWANDA VIDOGO VYA KUSINDIKA VYAKULA.
Reviewed by safina radio
on
March 22, 2018
Rating:
No comments