MAREKANI YATANGAZA KUWAFUKUZA WANADIPLOMASIA NCHINI HUMO.


Nchi ya Marekani pamoja na mataifa mengine manne kwenye umoja wa Ulaya wametangaza kuwafukuza  kwenye nchi zao wanadiplomasia wa Urusi baada ya tukio la kupewa sumu jasusi wa Urusi  jijini London majuma kadhaa yaliyopita.

Image result for PICHA YA RAIS TRUMP
Rais wa Marekani Donald Trump kwa upande wake ameagiza kufukuzwa nchini humo kwa maafisa 60 wanaodaiwa kuwa ni majasusi wa Urusi katika kile kinachoonekana ni kujibu mapigo kutokana na tukio la kupewa sumu kwa jasusi wake wa zamani mjini Salisbury.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje Sarah Sanders amesema hatua hiyo imetokana na juhudi za kidunia dhidi ya Urusi hatua zilizochukuliwa baada ya Urusi kudaiwa kutumia sumu yenye kemikali kwenye ardhi ya Uingereza.
Marekani inasema maofisa 48 ambao hawajulikani wako Marekani na wengine 12 kwenye umoja wa Mataifa na sasa wanazo siku 4 kuondoka Nchini Marekani.
Rais Trump pia ameagiza kufungwa kwa ofisi za ubalozi wa Urusi mjini Seattle, ofisi ambazo Marekani inasema zilikuwa zinatumiwa na Urusi kufanya ujasusi.
Katika hatua nyingine mataifa 14 ya  umoja wa Ulaya yanawafukuza wanadiplomasia wa Urusi katika kile kinachoonekana ni kuungana na nchi ya Uingereza dhidi ya Urusi inayotuhumiwa kutumia sumu dhidi ya jasusi wake wa zamani.

MAREKANI YATANGAZA KUWAFUKUZA WANADIPLOMASIA NCHINI HUMO. MAREKANI YATANGAZA KUWAFUKUZA WANADIPLOMASIA NCHINI HUMO. Reviewed by safina radio on March 27, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.