RAIS WA URUSI VLADIMIR PUTIN ANAJIANDAA KUONGOZA TAIFA HILO KWA MIAKA MINGINE SITA
Rais wa Urusi Vladmir Putin anajiandaa kuongoza taifa hilo kwa
miaka sita mingine baada ya kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu wa
rais ambao hadi sasa ni washirika wake wa karibu ndio waliompongeza wakati huu
uhusiano kati ya nchi yake na mataifa ya magharibi ukisuasua.
RAIS VLADMIR PUTIN WA URUSI |
Rais Putin ambaye ameitawala Urusi kwa karibu miongo miwili,
amepata ushindi wake wa kwanza mkubwa wa asilimia 76.67 ya kura zote lakini
akakanusha pia taarifa kwamba amepanga kuwa rais wa kudumu.
Upinzani unasema kuwa matokeo hayo yametengenezwa, ukidai kuwa
kuna masanduku ambayo kura ziliwekwa kabla, pamoja na matukio mengine ya
ukiukwaji wa sheria za uchaguzi.
Awali utawala wa Moscow ulikuwa umehamasisha wananchi kujitokeza
kwa wingi kwenye zoezi la upigaji kura katika kile kilichoonekana ni kujaribu
kuufanya uchaguzi huo uwe wa kuaminika.
Rais Putin ambaye sasa ataongeza muda wa utawala wake hadi mwaka
2024 tayari ni kiongozi aliyeoongoza taifa hilo kwa muda mrefu zaidi tangu
kumalizika kwa utawala wa Stalin.
RAIS WA URUSI VLADIMIR PUTIN ANAJIANDAA KUONGOZA TAIFA HILO KWA MIAKA MINGINE SITA
Reviewed by safina radio
on
March 19, 2018
Rating:
No comments