WAKULIMA GEITA WATAKIWA KUWA WAANGALIFU KWA MAZAO WANAYOYAPATA PAMOJA NA KUYATUMIA KWA FAIDA.


Wito umetolewa kwa wakulima wa kijiji cha Isamilo, wilayani Geita mkoani Geita, kuwa waangalifu kwa mazao wanayoyapata pamoja na  kuyatumia kwa faida.

Image result for Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Emili Kasagara
Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Geita Emily Kasagara.
Wito huo umetolewa na Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Geita Emily Kasagara, wakati wa mavuno ya pamoja ya mahindi ya mbegu ya mahindi aina ya    WEMA 2109 yaliyofanywa na wakulima wa kijiji cha Isamilo Wilayani Geita, Mkoani Geita.

Mavuno hayo ya pamoja yamefanyika katika moja ya shamba darasa wilayani Geita ambapo wakulima hao wamesema kuwa mbegu hizo zinastahimili ukame na kutoa mazao mengi.

Aidha, Wakulima hao wa Kijiji cha Isamilo wamepongeza mradi wa mbegu hiyo ya mahindi aina ya WEMA 2109 iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia COSTEC kwa kushirikiana na Jukwaa la Bio Teknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo-OFAM.

Hata hivyo, Mwaka jana Tume ya Sayansi na Teknolojia-COSTEC na Jukwaa la Bio Teknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo-OFAM walitoa mafunzo kwa maafisa ugani na baadae wakaenda kupanda mbegu katika shamba darasa mbali mbali mkoani Geita.


WAKULIMA GEITA WATAKIWA KUWA WAANGALIFU KWA MAZAO WANAYOYAPATA PAMOJA NA KUYATUMIA KWA FAIDA. WAKULIMA GEITA WATAKIWA KUWA WAANGALIFU KWA MAZAO WANAYOYAPATA PAMOJA NA KUYATUMIA KWA FAIDA. Reviewed by safina radio on March 23, 2018 Rating: 5

No comments