NAIBU WAZIRI WA KILIMO DK. MARY MWANJELWA AMESEMA USHARIKA NI CHOMBO PEKEE KINACHOWEZA KUMKOMBOA MKULIMA


SONGWE.

Naibu Waziri wa Kilimo Dk. Mary Mwanjelwa amesema usharika ndio chombo pekee kinachoweza kuleta ukombozi wa matokeo chanya kwa mkulima.

Naibu Waziri wa Kilimo Dk. Mary Mwanjelwa.

Dk. Mwanjelwa ameyasema hayo mkoani Songwe wakati akizungumza na wakulima wa Kahawa na wanunuzi wa zao hilo na amesisitiza kuwa kamwe serikali haiwezi kuwapa mwanya walanguzi wa mazao ya wakulima ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakijinufaisha kupitia jasho la mkulima.

Aidha, amesema serikali ya awamu ya tano inawapenda na kuwajali wakulima kwa wakati wote na imekuwa ikifanya mkakati wa kumwangali mkulima ili  aweze kunufaika kwa kiwango fulani.

Amesema kuwa wakulima lazima wapende vyama vya ushirika  kwa kuwa ni vyombo vinavyoweza kuwasaidia wakulima.

Hata hivyo, Baadhi ya wakulima wa Kahawa kutoka  wilaya za Mbozi na Ileje wamepongeza hatua ya serikali ya kufufua upya vyama vya ushirika jambo ambalo litakuwa na manufaa kwa wakulima.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO DK. MARY MWANJELWA AMESEMA USHARIKA NI CHOMBO PEKEE KINACHOWEZA KUMKOMBOA MKULIMA NAIBU WAZIRI WA KILIMO DK. MARY MWANJELWA AMESEMA USHARIKA NI CHOMBO PEKEE KINACHOWEZA KUMKOMBOA MKULIMA Reviewed by safina radio on March 06, 2018 Rating: 5

No comments