MKOA WA KIGOMA UNAKABILIWA NA UPUNGUFU WA WATUMISHI WA AFYA ZAIDI YA ELFU TATU
Imeelezwa kuwa mkoa wa Kigoma una upungufu wa
watumishi wa afya wapatao elfu tatu mia tatu arobaini na nne ikiwa ni upungu wa
asilimia 66 ya watumishi hao.
MH. KANDEGE NAIBU WAZIRI TAMISEMI |
Hayo yameelezwa na naibu waziri wa nchi ofisi ya
rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa Mh Josephat Kandege wakati akijibu
swali la mbunge wa viti maalumu mkoa wa Kigoma Mh Josephine Gezebuke aliyetaka
kujua ni lini serikali itapeleka watumishi wa afya katika hospitali za wilaya
na vituo vya afya katika mkoa huo.
Amesema kuwa kwa mujibu wa Ikama mpya ya serikali ya
mwaka wa 2014 mkoa wa Kigoma unataikiwa
kuwa na watumishi wa afya elfu tano na saba lakini walioko sasa ni elfu moja
mia sita sitini na tatu pekee sawa na asilimia 33.2
Ameongeza kuwa ili kukabiliana na changamoto hiyo
serikali ilijiwekea mipango mbalimbali ambapo katika mwaka wa fedha wa
2017/2018 mkoa wa Kigoma ulipatiwa watumishi wa afya 95 wakiwemo madaktari
5,matabibu 24 wauguzi 33 wafamasia 17 na wataalamu wa maabara 16.
Aidha naibu waziri Kandege amesema katika mwaka wa
fedha wa 2018/2019 serikali itaendelea
kupunguza tatizo hilo kwa kuajiri
watumishi wa afya wenye kada mbalimbali kwa kadri fedha
zitakavyopatikana.
Hata hivyo mkutano wa 11 wa bunge unaendelea bungeni
mjini Dodoma ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti za wizara mbalimbali
katika mwaka wa fedha wa 2018/2019.
MKOA WA KIGOMA UNAKABILIWA NA UPUNGUFU WA WATUMISHI WA AFYA ZAIDI YA ELFU TATU
Reviewed by safina radio
on
April 12, 2018
Rating:
No comments