ZAIDI YA WASICHANA ELFU THELATHINI WENYE UMRI WA MIAKA 14 KUPATIWA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI MKOANI SIMIYU
Jumla ya wasichana elfu thelethini na saba
mkoani Simiyu wenye umri wa miaka kumi
na nne wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya Saratani ya Mlango wa Kizazi.
Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa huo
Festus Shaga wakati akifungua mafunzo ya utoaji chanjo hiyo ambapo amesema kuwa
wadau wa afya wakiwemo vingozi wa vyama vya siasa na dini watatoa ushirikiano
ili kufanikisha zoezi hilo.
Kwa upande wake Mganga mkuu wa Mkoa wa Simiyu
Dkt. Mageda Kihulya amesema kuwa chanjo hiyo itasaidia kupunguza vifo vya
wanawake ambapo hupelekwa kwenye matibabu wakiwa na hali mbaya.
Hata hivyo, Mkoa wa Simiyu unatarajia kutoa
chanjo hiyo kuanzia tarehe 25 mwezi huu
ZAIDI YA WASICHANA ELFU THELATHINI WENYE UMRI WA MIAKA 14 KUPATIWA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI MKOANI SIMIYU
Reviewed by safina radio
on
April 17, 2018
Rating:
No comments