RAIS MAGUFULI ABADILISHA VYEO VYA MAAFISA NDANI YA JESHI LA WANANCHI TANZANIA JWTZ.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo Aprili 12, 2018 amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ katika vyeo mbalimbali.
Image result for rais magufuli
Rais Magufuli.
Taarifa hiyo ilisomwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Salvatory Mabeyo, Ikulu Jijini Dar es Salaam ambapo imeeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo Meja Jenarali Peter Paul Massao kuwa Luteni Jenerali ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Maafisa Wanafunzi wa Jeshi Monduli TMA na kwa uteuzi huo, sasa JWTZ itakuwa na Luteni Jenerali wawili.

Aidha, Mhe. Dk. Magufuli amempandisha cheo Brigedia Jenerali Henry Kamunde kuwa Meja Jenerali huku akiwapandisha vyeo maafisa 27 wa JWTZ kutoka cheo cha Kanali na kuwa Brigedia Jenerali na Afisa 1 kutoka Luteni Kanali na kuwa Kanali.
Hali kadhalika waliopandishwa vyeo hivyo ni D.D.M Mullugu, J.J Mwaseba, A.S Mwamy, R.K Kapinda, C.D Katenga, Z.S Kiwenge, M.A Mgambo, A.M Alphonce, A.P Mutta, A.V Chakila, M.G Mhagama, V.M Kisiri, C.E Msolla na S.M Mzee.
Wengine ni C.J Ndiege, I.M Mhona, R.C Ng’umbi, S.J Mnkande, A.C Sibuti, M.M Mumanga, I.S Ismail, M.N Mkeremy, G.S Mhidze, M.A Machanga, S.B Gwaya, P.K Simuli na M.E Gaguti.
Vile vile, Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo Luteni Kanali Bernard Masala Mlunga kuwa Kanali na ameteuliwa kuwa Mpambe wa Rais-AIDE DE CAMP – ADC akichukua nafasi ya Kanali Mbaraka Naziad Mkeremy ambaye amepandishwa cheo kuwa Brigedia Jenerali.

RAIS MAGUFULI ABADILISHA VYEO VYA MAAFISA NDANI YA JESHI LA WANANCHI TANZANIA JWTZ. RAIS MAGUFULI ABADILISHA VYEO VYA MAAFISA NDANI YA JESHI LA WANANCHI TANZANIA JWTZ. Reviewed by safina radio on April 12, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.