UGANDA ITAANZA KUTOA CHANJO YA KIPINDUPINDU BAADA YA VIFO VYA WATU 44 HUKU ZAIDI YA 2000 KULAZWA.
Wizara
ya afya nchini Uganda itaanza kutoa chanjo ya ugonjwa wa kipindupindu ili
kudhibiti mlipuko wa ugonjwa huo katika kambi za wakimbizi kutoka Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo DRC uliosababisha vifo vya watu 44 na wengine zaidi ya
elfu 2 kulazwa tangu mwezi Februari mwaka huu.
Uganda. |
Kaimu
mkurugenzi wa huduma za afya nchini humo Charles Olaro amesema, chanjo hiyo
imepangwa kuanza mwezi ujao na itatolewa katika kambi za wakimbizi za Kyangwali
na Kyaka II, ambazo ziko kwenye wilaya za magharibi za Hoima na Kyegegwa.
Bw.
Olaro amesema chanjo hiyo pia itatolewa katika maeneo mengine nchini Uganda
ikiwemo Buliisa, Pakwach, Kasese, na Zombo.
UGANDA ITAANZA KUTOA CHANJO YA KIPINDUPINDU BAADA YA VIFO VYA WATU 44 HUKU ZAIDI YA 2000 KULAZWA.
Reviewed by safina radio
on
April 17, 2018
Rating:
No comments