TATIZO LA MIGOGORO SUGU YA ARDHI SASA KUTATULIWA SINGIDA.
Tatizo sugu la migogoro ya mipaka baina ya vijiji,
kata na wilaya ya jirani na Halmashauri ya Itingi Mkoani Singida huenda
likatatuliwa baada ya kununuliwa kwa vifaa vya kisasa vinavyogharimu mamilioni
ya fedha zenye uwezo wa kubaini alama za mipaka ya zamani ili kuondoa utata.
Hayo yamebainika kwenye kikao cha kawaida cha baraza
la madiwani ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Pius Mhende na
Mtaalamu wa Upimaji Ardhi Juma Rashidi kupitia vifaa hivyo vya kisasa vyenye
thamani ya fedha shilingi milioni 54.
Madiwani wamekuwa na matumaini kuwa vifaa hivyo
vitamaliza migogoro ya ardhi,mipaka pamoja na kupima viwanja vya makazi ya watu
ili kuwezesha kutumia rasilimali hiyo kujikomboa kiuchumi.
Kabla ya kununuliwa kwa vifaa hivyo vyenye uwezo wa
kupima zaidi ya viwanja 100 kwa saa ishirini na nne halmashauri ya wilaya ya
Itigi ilikuwa ikodi vifaa hivyo kwa shilingi laki tatu kwa siku kwa kupima
makazi ya wananchi wake kwa lengo la kumaliza migogoro ya mipaka.
TATIZO LA MIGOGORO SUGU YA ARDHI SASA KUTATULIWA SINGIDA.
Reviewed by safina radio
on
April 26, 2018
Rating:
No comments