UINGEREZA, UFARANSA, UFARANSA NA UJERUMANI YAAHIDI KUUNGA MKONO MAKUBALIANO YA SASA YA NYUKLIA, IRAN.


Viongozi wa Uingereza , Ufaransa na Ujerumani wameahidi kuunga mkono makubaliano ya sasa ya nyukilia yaliyofikiwa mwaka 2015 kati ya Iran na mataifa makubwa yenye nguvu duniani.
 Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi ya waziri mkuu wa Uingereza viongozi wa nchi hizo tatu wamesema makubaliano hayo ni njia nzuri inayosaidia kupunguza kitisho cha silaha za nyukilia cha Iran.
Waziri Mkuu wa Uingereza  Theresa May alizungumza kwa simu na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron pamoja na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel mwishoni mwa wiki na viongozi hao wakakubaliana kuwa njia pekee ilikuwa ni kuyalinda makubaliano hayo yaliyotiwa saini mwaka 2015.
Hata hivyo rais Donald Trump wa Marekani amekuwa akitishia kujiondoa kwenye makubaliano hayo ambapo mwezi Mei huenda akafanya uamuzi.

UINGEREZA, UFARANSA, UFARANSA NA UJERUMANI YAAHIDI KUUNGA MKONO MAKUBALIANO YA SASA YA NYUKLIA, IRAN. UINGEREZA, UFARANSA, UFARANSA NA UJERUMANI YAAHIDI KUUNGA MKONO MAKUBALIANO YA SASA YA NYUKLIA, IRAN. Reviewed by safina radio on April 30, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.