TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA MAREKANI KATIKA NYANJA MBALIMBALI
Naibu waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa TAMISEMI Josephat Kandege amesema kuwa serikali ya Tanzania
itaendelea kushirikia na serikali ya Marekani katika Nyanja mbali mbali za
maendeleo zikiwemo elimu afya na kilimo.
NAIBU WAZIRI TAMISEMI JOSEPHAT KANDEGE |
Naibu Waziri Kandege ameyasema hayo mjini Morogoro
wakati wa kufunga mafunzo ya wiki mbili kwa vijana wa Marekani 52 waliopo
nchini kwa lengo la kujitolea utaalamu katika huduma mbali mbali za kijamii.
Kwa upande wake Meneja wa Mafunzo kutoka Shirika la
Huduma za kujitolea za Wamarekani USPSCOP Elance Ndilu amesema kuwa katika
mafunzo hayo vijana hao wamejifunza lugha ya Kiswahili pamoja na utamaduni na
watakaa nchini kwa muda wa miaka miwili.
TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA MAREKANI KATIKA NYANJA MBALIMBALI
Reviewed by safina radio
on
April 19, 2018
Rating:
No comments