RAIS MAGUFULI APANDISHA HADHI MANISPAA YA DODOMA KUWA JIJI.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo ametangaza
rasmi mkoa wa
Dodoma kuwa jiji
badala ya kuitwa
manispaa wakati akiwa mgeni
rasmi katika maadhimisho ya Sherehe za Miaka 54 ya Muungano wa Tanzania Bara na
Visiwani yanayofanyika katika uwanja wa Jamhuri jijini humo.
Mh.Magufuli
ametangaza Dodoma kuwa jiji ili kuinua hadhi ya
makao makuu ya nchi na
kuongeza idadi ya
majiji nchini sanjari na
kumtangaza aliyekuwa mkurugenzi wa mji
wa Dodoma kuanzia sasa
kuwa ataitwa mkurugenzi wa
jiji.
Aidha
mheshimiwa Rais ameagiza taasisi zinazohusika na mipango ya
majiji kuandaa mipango
yote ya kiserikali
kuhusu Dodoma sasa
yawe yanafanyika kwa kuzingatia
kuwa Dodoma ni jiji.
Vile vile
Rais Magufuli amesema
serikali ya jamhuri
ya muungano wa Tanzania italinda muungano kwa namna
yeyote na kamwe
haitamwonea aibu,huruma wala haya
mtu yeyote atakaye jaribu kuvunja
amani na muungano wa
jamhuri ya muungano
wa Tanzania.
Hata hivyo
mheshimiwa Rais pamoja
na kutangaza Dodoma
kuwa jiji amesema
kuwa mwaka huu
atahamia Dodoma .
RAIS MAGUFULI APANDISHA HADHI MANISPAA YA DODOMA KUWA JIJI.
Reviewed by safina radio
on
April 26, 2018
Rating:
No comments