ZOEZI LA UTOAJI WA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI WAANZA ARUSHA.


Kaimu mkuu wilaya ya Arumeru ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Monduli Bw. Idd Kimanta amesema kuwa serikali itachukua hatua kali za kisheria kwa  mtu yeyote Yule atakayejaribu kukwamisha zoezi la utoaji chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 14.
Image result for CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

Bw Kimanta ametoa kauli hiyo wakati akizindua zoezi la utoaji chanjo hiyo katika hospitali ya wilaya Tengeru ambapo amewataka viongozi wote wanaohusika wakiwemo wakuu wa shule,watendaji wa kata, maafisa elimu pamoja na wenye viti wa maeneo yote kusimamia vizuri zoezi hilo bila kuingiza kikwazo chochote.

Amesema kuwa serikali imekusudia kutoa chanjo hiyo ili kusaidia kinga ya maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi kwa kizazi kijacho hasa kwa wasichana wadogo hivyo serikali haitamvumilia mtu yeyote atakayekwamisha zoezi hilo.

Kwa upande wa mganga mkuu wa wilaya hiyo Dr Cosmas Kilasara amesema kuwa jumla  ya wanawake 5892 wamefanyiwa uchunguzi wa ugonjwa huo ambapo 319 waligundulika kuwa na dalili za awali huku 19 kati yao wakipatiwa rufaa ya kwenda hospitali ya Ocean road baada ya kugundulika kuwa saratani hiyo imesambaa zaidi mwilini.

ZOEZI LA UTOAJI WA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI WAANZA ARUSHA. ZOEZI LA UTOAJI WA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI WAANZA ARUSHA. Reviewed by safina radio on April 25, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.