SERIKALI YAOMBWA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA HUSUSANI KUONGEZA WATOA HUDUMA ZA AFYA.


Wakazi wa Kijiji cha Muguhesi Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma wameiomba serikali kuboresha huduma za afya ikiwa ni pamoja na kuongezwa kwa watoa huduma kwenye kituo cha afya kilichopo kijijini hapo.

Image result for wauguzi
Watoa huduma.

Ombi hilo wamelitoa katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo uliokutanisha kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Tunduru na Viongozi wa Kijiji.

Wakizungumza katika Mkutano wa Hadhara wakazi wa Kijiji hicho wamesema kuwa kituo hicho cha afya kina wauguzi wawili tu hali inayosababisha msongamano kutokana na wingi wa wagonjwa.

Naye Mkuu wa kituo hicho cha afya Esata Milanzi amesema kuwa kituo hicho kinahudumia zaidi ya vitongoji sita na kusababisha kuelemewa na wingi wa wagonjwa hasa wakinamama wajawazito.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Kohomera amekiri kuwepo kwa wingi wa wagonjwa katika kituo hicho hivyo ameahidi kulifanyia kazi ombi hilo huku kituo hicho kikiwa kinawahudumia zaidi ya wagonjwa 46 katika vitongoji zaidi ya sita.

SERIKALI YAOMBWA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA HUSUSANI KUONGEZA WATOA HUDUMA ZA AFYA. SERIKALI YAOMBWA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA HUSUSANI KUONGEZA WATOA HUDUMA ZA AFYA. Reviewed by safina radio on April 30, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.