KIGOMA SASA KUUNGANISHWA KATIKA GRIDI YA TAIFA KUTOKA KIGOMA.
Waziri wa Nishati Mh Dkt.Merdad Kalimani amesema
kuwa ili kukabiliana na tatizo la umeme kukatika mara kwa mara katika wilaya Kaliuwa
na Urambo mkoani Tabora na kuunganisha mkoa wa Kigoma kwenye Gridi ya Taifa Serikali
imetenga bilioni 10 kwa ajili ya kujenga vituo viwili vya kupooza na kuongeza umeme
katika mikoa hiyo.
![]() |
Dk. Merdad Kalimani. |
Akizungumza kwa nyakati tofauti katika wilaya za Kaliuwa
na Urambo waziri Kalimani amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo hautachukuwa muda
kuanza ambapo kituo kimoja kitajengwa mpakani mwa Kaliuwa na Urambo na kingine kitajengwa
mpakani mwa wilaya ya Kaliuwa na Uvinza.
Akiwa katika kijiji cha Jionee Mwenyewe Wilayani Urambo,
Waziri Kalimani amezindua mradi wa usambazaji wa umeme vijijni kwa kupitia
Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijni REA awamu ya tatu.
KIGOMA SASA KUUNGANISHWA KATIKA GRIDI YA TAIFA KUTOKA KIGOMA.
Reviewed by safina radio
on
April 18, 2018
Rating:

No comments