WAISRAEL LEO WAMEKAA KIMYA KWA MUDA KUKUMBUKA MAANGAMIZI YA WAYAHUDI MILIONI 6.


Wananchi wa Israel leo wamekaa kimya kwa muda kukumbuka maangamizi ya Wayahudi milioni sita katika mauaji ya halaiki ya Holocaust yaliyofanywa na wanazi miaka iliyopita.

Image result for mauaji ya halaiki ya Holocaust ya waisrael.
Mauaji ya halaiki ya Holocaust.

Ving’ora vimelia kwa dakika mbili kote nchini Israel kutoa heshima kwa wahanga wa mauaji hayo, ambapo Shughuli za kawaida nchini humo zimesimama kwa muda kwa ajili ya kumbukumbu hiyo.

Wakati huohuo Maelfu ya Wayahudi wanatarajiwa kuandamana leo kutoka iliyokuwa kambi ya mateso ya Eshwets hadi Beknau nchini Poland kama sehemu ya makumbusho hayo.

Rais wa Israel Reuven Rivlin atawaongoza takriban watu elfu kumi na mbili watakaoshiriki katika maandamano hayo ya Poland.

Wakati hayo yakijiri, Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameionya Iran kutoijaribu nchi yake, na kuilinganisha na utawala wa wanazi, akiongeza kuwa onyo lake siyo maneno matupu.

WAISRAEL LEO WAMEKAA KIMYA KWA MUDA KUKUMBUKA MAANGAMIZI YA WAYAHUDI MILIONI 6. WAISRAEL LEO WAMEKAA KIMYA KWA MUDA KUKUMBUKA MAANGAMIZI YA WAYAHUDI MILIONI 6. Reviewed by safina radio on April 12, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.