WANACHAMA 30 WA AL-SHABABU WAMEUAWA.


Wanachama 30 wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab lenye mfungamano na mtandao wa al-Qaeda wameuawa katika operesheni kali iliyotekelezwa na Jeshi la Taifa la Somalia katika eneo la Hiran jana Jumanne.
Image result for Wanachama 30 wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab wameuawa
Msemaji wa jeshi katika eneo hilo Mohammad Nur Agajof, amesema kuwa magaidi hao wameuawa katika operesheni ya jana Jumanne katika miji ya Beledwein, Mahas na Mataban katika eneo la Hiran, katikati ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
Amesema mbali na kuangamiza makumi ya wanamgambo hao, askari wa Somalia wameteka Kamandi Kuu ya magaidi hao katika eneo hilo, sanjari na kupata silaha za kijeshi zilizokuwa mikononi mwa wapiganaji hao wa Kitakfiri.
Haya yanajiri siku chache baada ya wanachama wa al-Shabaab kutekeleza shambulizi la kigaidi na kuwaua watu watano katika uwanja wa mpira wa miguu katika mji wa Pwani wa Barawa kusini mwa Somalia.
Kundi hilo limeanzisha hujuma zake nchini Somalia mnamo mwaka 2007 kwa lengo la kuiondoa madarakani serikali ya nchi hiyo kwa kile wanachokiita kuwa ni serikali ya kikafiri.

WANACHAMA 30 WA AL-SHABABU WAMEUAWA. WANACHAMA 30 WA AL-SHABABU WAMEUAWA. Reviewed by safina radio on April 18, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.