WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMEWATAKA MAWAZIRI NA MANAIBU MAWAZIRI KUACHA KUTOA MATAMKO YASIYOTEKELEZEKA.

08-11-2017


Waziri Mkuu Kasim Majaliwa amewataka Mawaziri na Manaibu Mawaziri kujiepusha na utoaji matamko yasiyotekelezeka ili kuepuka mikanganyiko serikalini.

Waziri Majaliwa ametoa kauli hiyo wakati akifungua kikao kazi cha baraza la Mawaziri kilichofanyika katika Ukumbi wa Hazina mjini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema kuwa kabla ya kutoa matamko ni vyema viongozi hao wakajiridhisha iwapo jambo hilo halitaleta athari kibajeti na kisera na kama lipo katika bajeti za wizara zao.

Aidha, Mh. Majaliwa amewataka viongozi hao kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya uongozi ili kithibitishia jamii kuwa wameteuliwa katika nafasi hizo kutokana na uwezo wao wa utendaji.


Vile vile, Waziri Mkuu amewataka Mawaziri kujiwekea utaratibu wa kusikiliza hoja na shida za wabunge na kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni.
WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMEWATAKA MAWAZIRI NA MANAIBU MAWAZIRI KUACHA KUTOA MATAMKO YASIYOTEKELEZEKA. WAZIRI  MKUU  KASSIM MAJALIWA  AMEWATAKA  MAWAZIRI NA  MANAIBU MAWAZIRI KUACHA  KUTOA MATAMKO  YASIYOTEKELEZEKA. Reviewed by safina radio on November 08, 2017 Rating: 5

No comments