NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI MH. JUMAA AWESO AMEWATAKA WAHANDISI WA MAJI KATIKA HALMASHAURI ZOTE KUSIMAMIA VYEMA MIRADI YA MAJI.

TAREHE 23-11-2017


Naibu waziri wa maji na umwagiliaji Mh Jumaa Aweso amewataka waandisi wa maji wa halmashauri zote hapa nchini kusimamia vyema miradi ya maji pamoja na jumuiya za watumia maji ili uwekezaji unaofanyika katika sekta hiyo uweze kuleta tija.

Mh Aweso ameyasema hayo muda mfupi baada ya kuzungumza na wafanyakazi na wanafunzi wa chuo cha maji jijini Dar-es-salaam,ambapo amesema kuwa upungufu  wa wataalamu wa maji elfu saba unasababisha kusuasua kwa baadhi ya miradi ya maji hapa nchini.

Amesema kuwa serikali inazitaka jumuiya zote zinazohusika na masuala ya miradi ya maji, lazima ziwe zimesajiliwa pamoja na kuwa na mfumo mzuri wa matumizi mazuri ya fedha katika miradi ya maji na kuepuka ubadhirifu unaoweza kujitokeza.

Naibu waziri huyo ameongeza kuwa ili kuhakikisha fedha za maji zinazopelekwa katika halmashauri hizo zinatumika kama ilivyopangwa ni lazima wahandisi wote wa halmashauri hizo wasimamie na kutoa elimu kwa jumuiya zote na hiyo itasaidia miradi ya maji inayotekelezwa na serikali kukaa kwa muda mrefu na kuwahudumia wananchi kama ilivyokusudiwa.


Naye mkuu wa chuo cha maji Dr Shija Kazumba amesema kuwa chuo chake kinakabiliwa na upungufu wa watumishi hali inayofanya chuo hicho kushindwa kutimiza majukumu yake kama ipasavyo.
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI MH. JUMAA AWESO AMEWATAKA WAHANDISI WA MAJI KATIKA HALMASHAURI ZOTE KUSIMAMIA VYEMA MIRADI YA MAJI. NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI MH. JUMAA AWESO  AMEWATAKA  WAHANDISI  WA  MAJI  KATIKA  HALMASHAURI  ZOTE  KUSIMAMIA VYEMA MIRADI YA MAJI. Reviewed by safina radio on November 23, 2017 Rating: 5

No comments