IDADI YA WALIOFARIKI KATIKA TETEMEKO NCHINI IRANI YAFIKA 350
TAREHE 14-11-2017
Idadi ya watu
waliokufa kutokana na tetemeko la ardhi katika mpaka wa Iran na Iraq, imefikia
350.
Wizara ya mambo ya
ndani ya Iran imesema watu wengine elfu sita na mia sita wamejeruhiwa na tetemeko hilo lililotokea jana
jioni na lililokuwa na ukubwa wa 7.3 katika kipimo cha Richta,huku majimbo ya Iran ya Kermansha na Illam ndiyo
yameathiriwa vibaya na tetemeko hilo la ardhi.
Msemaji wa shirika la
kukabiliana na majanga nchini Iran, Behnam Saeedi amesema waliojeruhiwa
wamepelekwa kwenye vituo vya matibabu.
Kituo cha Marekani kinachohusika na utafiti wa
kijiolojia, kimesema eneo kuu la tetemeko hilo lilikuwa kwenye mkoa ulioko
milimani nchini Iraq, umbali wa kilomita mia mbili kaskazini mashariki mwa Baghdad na kilomita mia
nne magharibi mwa Tehran.
IDADI YA WALIOFARIKI KATIKA TETEMEKO NCHINI IRANI YAFIKA 350
Reviewed by safina radio
on
November 14, 2017
Rating:

No comments