MKUU WA MKOA WA PWANI EVARIST NDIKILO AWAAGIZA WAKUU WOTE WA WILAYA MKOANI HUMO KUPIGA MARUFUKU UTOROSHWAJI WA KOROSHO.

TAREHE 1-11-2017

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo amewaagiza Wakuu wa Wilaya zote mkoani  humo kupiga marufuku utoroshwaji wa zao la Korosho unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara ambao  wanahujumu   uuzwaji wa zao hilo kwa kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani.

Mhandisi Ndikilo ametoa agizo hilo wilayani Mkuranga mkoani humo wakati wa kikao cha Bodi ya Korosho na kuongeza kuwa hatua ya wafanyabiashara hao kuhujumu mfumo huo inamkandamiza mkulima.


Hata hivyo baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Korosho Mkoani Pwani mbali na kupongeza juhudi za serikali za kuboresha upatikanaji wa pembejeo na dawa ya Salfa pia wamelalamikia upatikanaji wa magunia yanayofaa kuhifadhia zao hilo.
MKUU WA MKOA WA PWANI EVARIST NDIKILO AWAAGIZA WAKUU WOTE WA WILAYA MKOANI HUMO KUPIGA MARUFUKU UTOROSHWAJI WA KOROSHO. MKUU  WA  MKOA  WA  PWANI  EVARIST  NDIKILO  AWAAGIZA WAKUU WOTE  WA  WILAYA MKOANI  HUMO  KUPIGA  MARUFUKU UTOROSHWAJI  WA KOROSHO. Reviewed by safina radio on November 01, 2017 Rating: 5

No comments