RAIS WA NIGERIA AWAFUKUZA KAZI MAAFISA WAWILI KWA TUHUMA ZA RUSHWA
TAREHE 31-10-2017
Rais
wa Nigeria, Muhammadu Buhari amewafukuza kazi maafisa wawili wa ngazi ya juu wa
serikali kwa tuhuma za kuhusika na rushwa, miezi sita baada ya kuwasimamisha
kazi.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Nigeria, Balozi Ayo Oke amefukuzwa kazi kwa tuhuma
za kujipatia fedha taslimu zaidi ya Dola za Kimarekani milioni 43.
Naye
afisa wa ngazi ya juu wa umma na katibu wa baraza la mawaziri, Babachir Lawal,
amefukuzwa kazi baada ya kutuhumiwa kubadilisha matumizi ya fedha za miradi ya
misaada zilizopangwa kutumika kwenye maeneo ambayo yameharibiwa na wanamgambo
wa kundi la Boko Haram.
Rais Buhari
aliyechaguliwa mwaka 2015, aliahidi kupambana na rushwa, lakini vyama vya
upinzani vinamshutumu kwa kuwalenga zaidi wapinzani wake kisiasa.
RAIS WA NIGERIA AWAFUKUZA KAZI MAAFISA WAWILI KWA TUHUMA ZA RUSHWA
Reviewed by safina radio
on
October 31, 2017
Rating:

No comments