MKUU WA MKOA WA ARUSHA BW. MRISHO GAMBO AMEWAOMBA WADAU MBALIMBALI KUMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI.

TAREHE 24-10-2017

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo amewaomba wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono jitihada za Mh. Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa vifaa vya ujenzi ili kuweza kukamilisha ujenzi wa nyumba za askari zilizoungua hivi karibuni. 

Bw Gambo ameyasema hayo leo alipotembelea ujenzi wa nyumba hizo unaoendelea katika kata ya Sekei ambapo amewashukurù wadau waliojitolea mpaka sasa na kuwaomba wengine kujitokeza katika kusaidia vifaa mbalimbali ili askari hao waweze kuishi kwenye mazingira mazuri. 

Aidha Gambo amemshukuru mwenyekiti wa kamati ya ujenzi kwa upande wa wadau binafsi Bw. Hans Paul kwa kuacha shughuli zake na kujitoa kusimamia ujenzi huo.

Pia amemshukuru raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kwa kuanzisha mchakato wa ujenzi wa nyumba hizo ambapo tarehe 16 mwezi wa tisa baada ya nyumba hizo kuteketea kwa moto alitoa kiasi cha shilingi milioni mia mbili sitini.

Hata hivyo kufikia sasa wadau mbalimbali wamejitokeza kutoa misaada mbalimbali ikiwemo vyakula, saruji, mabati na fedha ambapo mpaka sasa nyumba hizo zenye uwezo wa kuhîfadhi familia 33  zimefikia hatua ya lenta. 
MKUU WA MKOA WA ARUSHA BW. MRISHO GAMBO AMEWAOMBA WADAU MBALIMBALI KUMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI. MKUU  WA  MKOA  WA  ARUSHA  BW.  MRISHO  GAMBO  AMEWAOMBA  WADAU  MBALIMBALI  KUMUUNGA  MKONO  RAIS  MAGUFULI. Reviewed by safina radio on October 24, 2017 Rating: 5

No comments