MAELFU WAANDAMANA HUKO BARCELONA KUPINGA CATALONIA KUJITENGA
TAREHE 09-10-2017
Mamia
kwa maelfu ya watu wamemiminika katika mitaa ya mji mkuu wa Catalonia,
Barcelona wameandamana wakipinga jimbo hilo kujitenga kutoka Uhispania na
kuonyesha ni kwa namna gani mkoa huo umegawanyika kuhusu suala hilo.
Polisi
wa ndani wamekadiria kwamba waandamanaji elfu thelathini na tano waliokuwa wamebeba bendera ya Uhispania na
Catalonia na mabango yaliyokuwa na ujumbe kwamba Catalonia ni Uhispania na
pamoja tuna nguvu, wameshiriki maandamano hayo.
Maandamano
hayo ya mjini Barcelona yaliandaliwa na
kundi linalopinga mkoa huo kujitenga la Catalan Civil society ili kuhamasisha
kile wanachoamini ni idadi kubwa ya walio kimya wanaopinga suala la kujipatia
uhuru.
MAELFU WAANDAMANA HUKO BARCELONA KUPINGA CATALONIA KUJITENGA
Reviewed by safina radio
on
October 09, 2017
Rating:

No comments