POLISI NCHINI MAREKANI KUFANYA UCHUNGUZI WA VIFO VYA WATU ZAIDI YA 59
TAREHE 03-10-2017
Baadhi ya wachunguzi wamedai mtu huyo kuwa na matatizo ya kisaikolojia lakini hilo bado halijathibitishwa.
Polisi wanajaribu kugundua sababu ya
ufyatuaji mkubwa wa risasi uliosababisha vifo vya watu 59 na kuwajehi wengine
527 kwenye warsha moja huko Las Vegas nchini Marekani.
Mtu mwenye silaha Stephen Paddock, mwenye
umrii wa miaka 64, alifyatua risasi kutoka ghorofa ya 32 ya hoteli ya Mandalay
Bay,wakati warsha moja ya mziki Jumapili ukiendelea usiku huko nchini Marekani.
Polisi walipata bunduki 23 kwenye
chumba chake cha hoteli na zingine 19 na vilipuzi nyumbani kwake huko Nevada lakini
hadi sasa hakuna sababu ya hatua yake hiyo iliyoibuka.
Wachunguzi hawajapata uhusiano
wowote na ugaidi licha ya kundi la Islamic State kudai kuhusika.
Baadhi ya wachunguzi wamedai mtu huyo kuwa na matatizo ya kisaikolojia lakini hilo bado halijathibitishwa.
POLISI NCHINI MAREKANI KUFANYA UCHUNGUZI WA VIFO VYA WATU ZAIDI YA 59
Reviewed by safina radio
on
October 03, 2017
Rating:

No comments