MUUNGANO WA UPINZANI NCHINI KENYA WAAHIRISHA MAANDAMANO NCHINI HUMO
TAREHE 7-10-2017
Muungano wa
upinzani nchini Kenya National Super Alliance (Nasa) umefutilia mbali maandamano
ambayo yalikuwa yamepangwa kufanyika leo nchini humo kushinikiza mageuzi katika tume ya
uchaguzi.
Muungano huo, kupitia taarifa, umesema
umechukua hatua hiyo kupata fursa ya kuomboleza watu ambao wameuawa kwenye
maandamano ya awali,ambapo maandamano hayo yataendelea tena siku ya Jumatano.
Nasa, muungano unaoongozwa na waziri mkuu
wa zamani Raila Odinga, ulikuwa umeahidi kufanya maandamano kila siku
kushinikiza mageuzi katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kabla ya
kufanyika kwa uchaguzi wa marudio.
MUUNGANO WA UPINZANI NCHINI KENYA WAAHIRISHA MAANDAMANO NCHINI HUMO
Reviewed by safina radio
on
October 17, 2017
Rating:

No comments