WAZIRI WA MALI ASILI NA UTALII DK. KIGWANGALA AMEITAKA MAMLAKA YA NGORONGORO KUKAA NA WAFUGAJI
TAREHE 27-10-2017
Waziri wa
Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangala ameagiza Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro kukaa pamoja na Wafugaji wa Ngorongoro ili kuhakikisha wanamaliza
migogoro na changamoto zote zinazowakabili wananchi wa eneo hilo.
Dk.
Kigwangala ameyasema wakati akizungumza na Watendaji pamoja na wajumbe wa
Baraza la Wafanyakazi katika Mamlaka hiyo,ambavyo amesema kuwa ni vyema Wafanyakazi
wakashirikiana ili kuhakikisha wana uhusiano wa karibu katika utendaji kazi
badala ya Kulaumiana.
Kwa upande
wke Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Dk. Fredy Manongi amesema
watahakikisha wanakutana na Baraza la Wafugaji la Ngorongoro na kujadili
masuala muhimu ya kisera ili kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.
WAZIRI WA MALI ASILI NA UTALII DK. KIGWANGALA AMEITAKA MAMLAKA YA NGORONGORO KUKAA NA WAFUGAJI
Reviewed by safina radio
on
October 27, 2017
Rating:

No comments