MAREKANI YAITAKA CUBA KUWAONDOA WAFANYAKAZI 15 KATIKA UBALOZI WAKE JIJINI WASHINGTON


TAREHE-10-2017
WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA MAREKANI REX TILLERSON
Marekani imeitaka Cuba kuondoa wafanyakazi 15 wa ubalozi wake mjini Washington kwa muda usiozidi siku saba, kufuatia madai kuwa Cuba imekuwa ikifanya mfululizo wa mashambulizi ambayo yaliathiri afya za wanadiplomasia 22 wa Marekani nchini Cuba mnamo miezi ya hivi karibuni.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Rex Tillerson amesema hatua hiyo ya Marekani imechukuliwa kutokana na kushindwa kwa Cuba kutilia maanani utaratibu wa kuwalinda wanadiplomasia wa nchi yake.


Wakati huo huo, Marekani ilitangaza Ijumaa iliyopita kuwa inaondoa theluthi mbili ya wafanyakazi wa ubalozi wake mjini Havana, na imetoa tahadhari kwa wamarekani wanaotaka kusafiri kuelekea kisiwani Cuba.
MAREKANI YAITAKA CUBA KUWAONDOA WAFANYAKAZI 15 KATIKA UBALOZI WAKE JIJINI WASHINGTON MAREKANI   YAITAKA CUBA  KUWAONDOA   WAFANYAKAZI  15  KATIKA UBALOZI WAKE  JIJINI WASHINGTON Reviewed by safina radio on October 04, 2017 Rating: 5

No comments