RAIS WA ZANZIBAR DR. ALL MOHAMED SHEIKN KUFUNGUA MKUTANO WA SIKU MBILI WA WADAU WA KILIMO JIJINI ARUSHA

TAREHE 04-10-2017
RAIS WA ZANZIBAR  DR. ALL  MOHAMED SHEIKN

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dr All Mohamed Sheikn anatarajiwa kufungua mkutano wa siku mbili wa  kimataifa wa wadau wa kilimo cha mboga mboga,matunda na maua utakaofanyika jijini Arusha.

Hayo yamesemwa na meneja mkuu (maendeleo ) kutoka Asasi ya kilimo cha   mboga mboga,matunda na maua (TAHA) ya jijini  Arusha Bw  Antony Chamanga wakati akizungumza na vyombo vya habari kuhusiana na mkutano huo unaotarajiwa kuanza october  9 mwaka huu jijini Arusha.

Chamanga amesema kuwa katika mkutano huo ambao utakuwa wa kimataifa  wadau wa sekta hiyo wataweza kujadili na kukubaliana maswala ya msingi ya kuendeleza sekta ya kilimo ikiwemo namna ya kuwafanya wakulima waweze kuzitambua teknolojia mpya za kisasa  ambazo zitawawezesha waweze kuongeza uzalishaji katika kilimo chao.

 Pia katika mkutano huo wadau hao wataangalia na kujadili ufikiaji wa masoko ya mazao hayo ya mboga mboga kwani masoko ni  moja ya changamoto inayowakabili wakulima wa sekta hiyo hivyo wadau kutoka taasisi mbambali wataweza kutoa uzoefu  kwa wakulima wauze wapi mazao yao na namna ya kuweza  kufikia fursa za masoko zilizopo nje ya nchi na hata ndani ya nchi.


Hata hivyo zaidi ya wadau 200 wa sekta ya kilimo  hapa nchini   wanatarajiwa kushiriki katika mkutano huo.
RAIS WA ZANZIBAR DR. ALL MOHAMED SHEIKN KUFUNGUA MKUTANO WA SIKU MBILI WA WADAU WA KILIMO JIJINI ARUSHA RAIS  WA  ZANZIBAR  DR. ALL  MOHAMED  SHEIKN   KUFUNGUA  MKUTANO   WA  SIKU  MBILI  WA  WADAU  WA  KILIMO   JIJINI  ARUSHA Reviewed by safina radio on October 04, 2017 Rating: 5

No comments