GEORGE WEAH AZIDI KUONGOZA KATIKA UCHAGUZI WA LIBERIA

13-10-2017

Tume ya uchaguzi nchini Liberia inasema mchezaji wa zamani wa kimataifa wa kandanda George Weah anaongoza katika matokeo ya awali ya wa rais nchini humo huku makamu wa rais Joseph Boakai naye pia akiongoza katika mkoa anakotoka huku matokeo hayo yakionesha kura katika maeneo mengi hazijahesabiwa.

Hata hivyo Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini humo Jerome Korkoya ametahadharisha kuwa matokeo hayo ya awali ya urais yanayoonesha mgombea wa chama cha Congress for Democtaric Change George Weah kuwa anaoongoza ni ya sehemu ndogo tu kati ya vituo vyote vya kupigia kura nchini humo.

Wafuasi wa mgombea wa tatu kwenye kinyanganyiro hicho wamekuwa wakidai kuwa kumekuwepo na kasoro katika uchaguzi huo huku vyama vya siasa vikionesha wasiwasi juu ya kasoro ambazo zimechangia kuchelewa kutangazwa kwa matokeo.


Hata hivyo Novemba 7 mwaka huu ndiyo siku iliyopangwa kufanyika uchaguzi wa marudio iwapo hakuna mgombea atakayeshinda kwa kiwango cha asilimia 50 cha kura za urais miongoni mwa wagombea 20 wanaowania nafasi hiyo.
GEORGE WEAH AZIDI KUONGOZA KATIKA UCHAGUZI WA LIBERIA GEORGE WEAH AZIDI KUONGOZA KATIKA UCHAGUZI WA LIBERIA Reviewed by safina radio on October 13, 2017 Rating: 5

No comments