CHUO KIKUU NCHINI KENYA CHAFUNGWA KWA MUDA USIOJULIKANA
TAREHE 04-10-2017
Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya kimefungwa kwa
muda usiojulikana, kufuatia maandamano ya wanafunzi dhidi ya ukatili wa polisi.
Naibu mkuu wa chuo hicho Peter Mbithi amesema
kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, kwamba kufungwa huko kumetokana na
kuzidi kuzorota kwa hali ya usalama, akiongeza kuwa wanafunzi 26 walikuwa
wamejeruhiwa na polisi walioingia chuoni, na kutumia gesi ya kutoa machozi
kuwatawanya waliokuwa wakiandamana.
Maandamano hayo yalianza wiki iliyopita, baada ya kukamatwa kwa
aliyewahi kuwa rais wa wanafunzi wa chuo kikuu hicho cha Nairobi Babu Owino,
ambaye alikuwa ameshinda kinyang'anyiro cha ubunge, akimuunga mkono kiongozi wa
upinzani Raila Odinga.
Hata hivyo Bw Odinga atapambana tena na Rais Uhuru
Kenyatta katika uchaguzi mpya wa rais utakaofanyika Octoba 27 mwaka huu, baada
ya matokeo ya uchaguzi wa kwanza kubatilishwa na mahakama kuu.
CHUO KIKUU NCHINI KENYA CHAFUNGWA KWA MUDA USIOJULIKANA
Reviewed by safina radio
on
October 04, 2017
Rating:

No comments