BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA KUPIGA KURA LEO JUU YA MASHAMBULIZI YA KEMIKALI NCHINI SYRIA.
TAREHE 24-10-2017
Baraza la
Usalama la Umoja wa Mataifa, linatarajiwa kupiga kura leo, juu ya kupanua
uchunguzi wa nani alihusika na mashambulizi ya silaha za kemikali nchini Syria.
Msemaji wa
Umoja wa Mataifa amethibitisha kuwa wajumbe wa baraza hilo watapigia kura,
azimio la kurefusha muda wa kamati ya pamoja ya uchunguzi ilioidhinishwa na
baraza hilo, pamoja na ujumbe wa kutafuta ukweli wa shirika la kuzuwia kuenea
kwa silaha za kemikali OPCW, kwa mwaka mwingine mmoja.
Mwaka 2013,
Baraza la Usalama lilipitisha azimio linaloitaka Syria kuharibu silaha zake za
kemikali na kukomesha mashambulizi kama hayo.
Zaidi ya
watu 80 waliuawa katika shambulizi la gesi ya sarin katika mji wa waasi mwezi
Aprili, ambalo wachunguzi wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, wanaoendesha
uchunguzi tofauti, wanasema lilifanywa na jeshi la anga la Syria.
BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA KUPIGA KURA LEO JUU YA MASHAMBULIZI YA KEMIKALI NCHINI SYRIA.
Reviewed by safina radio
on
October 24, 2017
Rating:

No comments