SERIKALI MKOANI MOROGORO KUWACHUKULIA HATUA WATUMISHI WATAKAOHUJUMU RUZUKU YA PEMBEJEO
TAREHE 19-10-2017
Serikali
mkoani Morogoro imesema haitasita kuwachukulia hatua kali watumishi wote
kuanzia ngazi ya kijiji hadi Mkoa watakaobainika kuhujumu ruzuku ya pembejeo za
kilimo na kusababisha hasara kwa wakulima na serikali.
Mkuu wa Mkoa
wa Morogoro Mh. Dk. Kebwe Stivin Kebwe ametoa onyo hilo wakati akitoa taarifa
kwa vyombo vya habari kuhusu hali ya chakula kwa mkoa huo kwa 2016-2017
Aidha,
Dk. Kebwe amesema kuwa wamefanya mawasiliano na wizara ya kilimo kupata orodha
ya watu waliofanya uhujumu katika pembejeo, ili kuwachukulia hatua huku akitoa
agizo kwa wakurugenzi wote wa halmashauri za mkoa huo wachukue hatua kwa
wasimamizi wote wa pembejeo waliofanya vitendo hivyo.
Vile
vile, Dk. Kebwe ameongeza kuwa kutokana na kero ya soko la mbaazi serikali ya mkoa
huo imeshampata mwekezaji atakaye jenga
kiwanda kikubwa cha kusaga zao hilo huku akiwaonya wananchi kutokutumia mazao
kwa matumizi yasiofaa ikiwemo kwenye ngoma na pombe.
SERIKALI MKOANI MOROGORO KUWACHUKULIA HATUA WATUMISHI WATAKAOHUJUMU RUZUKU YA PEMBEJEO
Reviewed by safina radio
on
October 19, 2017
Rating:

No comments