MAREKANI YAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA NA KOREA KUSINI
TAREHE 11-10-2017
Marekani kwa mara
nyingine imefanya mazoezi ya kijeshi kwa pamoja na Korea Kusini, ambapo ndege
zake mbili za kivita za kuangusha mabomu zimepaa juu ya rasi ya Korea.
Ndege hizo za kutekeleza mashambulizi aina
ya B-1B zimepaa angani pamoja na ndege za kivita za Korea Kusini aina ya F-15K.
Ndege hizo zimefanya mazoezi ya kurusha makombora kutoka angani
hadi ardhini katika maji ya bahari ya Korea Kusini.
Mazoezi hayo yamefanyika huku wasiwasi na
uhasama kati ya Marekani na Korea Kaskazini kuhusu mpango wake wa nyuklia
ukizidi.
Pyongyang ilitekeleza jaribio lake la sita la silaha za
nyuklia na pia imerusha makombora kupitia anga ya Japan mara mbili miezi ya
karibuni.
Jeshi la Korea Kusini limesema Ndege hizo
za Marekani zilipaa kutoka kisiwa chake cha Guam katika Bahari ya Pacific
Jumanne usiku, kabla ya kuingia anga ya Korea Kaskazini na kufanya mazoezi
katika Bahari ya Mashariki na Bahari ya Manjano.
Hata hivyo ikulu ya White House
imesema Rais wa Marekani Donald Trump
alikutana na maafisa wakuu wa usalama Jumanne usiku kujadili njia za kukabili
vitisho vya Korea Kaskazini.
MAREKANI YAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA NA KOREA KUSINI
Reviewed by safina radio
on
October 11, 2017
Rating:

No comments