MADEREVA MKOANI ARUSHA WATAKIWA KUTII SHERIA ZA USALAMA BARABARANI
TAREHE 02-10-2017
Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Arusha
Bw Nuru Seleman amewataka madereva kuheshimu na kutii sheria za usalama wa
barabarani ili kuepukana na ajali
zinazoweza kuzuilika.
Bw Selemani ametoa kauli hiyo jijini Arusha wakati akizungumza
na wananchi pamoja na wanafunzi waliojitokeza katika maadhimisho ya siku ya
SUMATRA iliyoandaliwa na baraza la ushauri la mamlaka ya usafiri wa majini na
nchi kavu Tanzania.
Amesema kuwa jeshi la polisi halitawavumilia
madereva wanaovunja sheria za usalama barabarani,na moja ya hatua
watakazochukuliwa kuwa ni pamoja na kufutiwa leseni zao,ambapo pia amelishukuru
baraza la ushauri la mamlaka ya usafiri wa majini na nchi kavu SUMATRA kwa
kuanzisha vilabu vya wanafunzi vinavyosaidia kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu
wa matumizi bora ya vyombo vya usafiri
Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza hilo mkoa wa
Arusha ameishukuru serikali kwa ushirikiano wanaoutoa kwa baraza hilo,ambapo
pia ametumia maadhimisho hayo kumuomba mkuu huyo wa usalama barabarani kusaidia
kusimamia zoezi la utoaji tiketi ili abiria aweze kupata haki yake pale tatizo
litakapotokea.
MADEREVA MKOANI ARUSHA WATAKIWA KUTII SHERIA ZA USALAMA BARABARANI
Reviewed by safina radio
on
October 02, 2017
Rating:

No comments