SERIKALI YATENGA FEDHA ILI KUWAPATIA VIJANA UJUZI KUHUSU UWEKEZAJI

TAREHE 19-10-2017
MH.JENISTA MUHAGAMA

Waziri wa Kazi Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mh. Jenista Muhagama amesema serikali imetenga fedha kwa ajili ya kuwapatia ujuzi vijana kuhusu uwekezaji wa viwanda ili kufikia uchumi wa kati.

Mh. Muhagama ameyasema hayo jijini Arusha wakati akifungua mkutano wa 7 wa Wadau wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF.

Aidha, Mh. Muhagama amesema kuwa lengo la kuwapatia ujuzi vijana hao linatokana na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kuwekeza katika viwanda 27 na kutoa ajira laki tatu.

Waziri Muhagama amewahakikishia wadau hao kuwa serikali imejipanga kulipa madeni yote ambayo  inadaiwa na  amewataka waajiri walipe michango, madeni, na malimbikizo yao.

Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Mikopo ya NSSF Prof. Samwel Wangwe amesema wameanzisha utaratibu kuwapokea askari wa Jeshi la Ulinzi wa Tanzania ili wanufaike kupata matibabu yao na familia zao.


Kwa upande wake Naibu Waziri wa wizara ya Kazi, Ajira Na Vijana Anthon Mavunde amesema kuwa suala la wanachama kujitoa katika Mifuko ya hifadhi ya Jamii ni changamoto inayoikabili Mifuko hiyo.
SERIKALI YATENGA FEDHA ILI KUWAPATIA VIJANA UJUZI KUHUSU UWEKEZAJI SERIKALI   YATENGA   FEDHA  ILI  KUWAPATIA   VIJANA  UJUZI  KUHUSU  UWEKEZAJI Reviewed by safina radio on October 19, 2017 Rating: 5

No comments