WAKENYA WANAPIGA KURA LEO KUMCHAGUA RAIS

TAREHE 26-10-2017

Wananchi wa kenya leo wanashiriki katika zoezi la kupiga kura ya urais katika uchaguzi mpya baada ya mahakama ya juu ya nchini humo kuubatilisha ushindi wa rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa mwezi Agosti mwaka huu.

Kiongozi wa muungano wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amewahimiza wafuasi wake kutoshiriki katika uchaguzi huo wa leo na hali ya wasiwasi imetanda huku ikihofiwa kwamba huenda kukazuka vurugu.

Wafuasi wa rais Uhuru Kenyatta, ambaye anawania awamu ya pili ya uongozi wa taifa la Kenya hapo jana walisherehekea pale walipopata habari kwamba zoezi la kupiga kura litaendelea baada ya Mahakama ya juu kushindwa kuendelea kusikiliza na kutoa maamuzi ya kusitisha kura hiyo.

Rais Uhuru Kenyatta amesema hali ya usalama itaimarishwa nchini kote na amewataka Wakenya kwenda kupiga kura huku wakizingatia haki za wale ambao hawataki kushiriki katika upigaji kura.
WAKENYA WANAPIGA KURA LEO KUMCHAGUA RAIS WAKENYA  WANAPIGA  KURA LEO KUMCHAGUA RAIS Reviewed by safina radio on October 26, 2017 Rating: 5

No comments