UELEWA MDOGO KUHUSU MASUALA YA LISHE WASABABISHA KUWEPO UTAPIA MLO.

TAREHE 16-10-2017


Imeelezwa kuwa uelewa mdogo wa masuala ya lishe miongoni mwa wananchi na viongozi umeendelea kuwa changamoto katika kukabilina na utapia mlo kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano nchini.

Hayo yameelezwa na mtaalamu wa Lishe kutoka ofisi ya rais TAMISEMI  Bw Muta Waibe katika uzinduzi wa mpango wa uongezaji wa virutubishi kwenye unga ambao unalenga kupunguza matatizo ya utapiamlo pamoja na udumavu kwa watoto na akinamama wote wenye umri wa kujifungua uliofanyika huko mkoani Iringa.

Aidha, Bw. Waibe ameeleza kuwa kutokana na serikali pamoja na wadau kutowekeza katika elimu ya lishe kumesababisha kuwa na kizazi kisichokuwa na uelewa wa mambo hivyo mikakati ya maendeleo yaliyopangwa kwa muda mrefu kukwama kutokana na kufanya mambo kinyume.

Kwa upande wake mkurugenzi Msaidizi wa mradi wa kuongeza virutubisho wa nafaka James Lock amesema mradi huo unatoa ruzuku kwa wasindikaji wa kati wenye uwezo wa kuzalisha hadi tani kumi kwa siku.


Hata hivyo virutubishi vinnavyoongezwa ni pamoja vile vya madini ya chuma, madini ya joto, protini, na vitamin B, ambavyo kukosekana kwake kunasababisha udumavu, utapia mlo, mgongo wazi pamoja na vichwa vikubwa.
UELEWA MDOGO KUHUSU MASUALA YA LISHE WASABABISHA KUWEPO UTAPIA MLO. UELEWA  MDOGO  KUHUSU   MASUALA   YA  LISHE  WASABABISHA KUWEPO  UTAPIA MLO. Reviewed by safina radio on October 16, 2017 Rating: 5

No comments