SERIKALI IMELIPA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI MIA MOJA NA TISINI IKIWA NI MADENI YA WAKANDARASI NA WAZABUNI.
TAREHE 18-10-2017
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Ashantu Kijaji amesema kuwa Serikali imekwisha lipa madeni ya wazabuni, wakandarasi na malimbikizo ya wafanyakazi yanayofikia kiasi cha Shillingi bilioni mia moja na tisini katika kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi septemba mwaka huu baada ya kufanya uhakiki wa madeni mbalimbali inayodaiwa.
![]() |
NAIBU WAZIRI WA FEDHA DK. ASHANTU KIJAJU |
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Ashantu Kijaji amesema kuwa Serikali imekwisha lipa madeni ya wazabuni, wakandarasi na malimbikizo ya wafanyakazi yanayofikia kiasi cha Shillingi bilioni mia moja na tisini katika kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi septemba mwaka huu baada ya kufanya uhakiki wa madeni mbalimbali inayodaiwa.
Dk.
Kijaji ameyasema hayo mjini Bukoba wakati akizungumza na Jumuiya ya Wafanyakazi
wa mkoa wa Kagera katika ziara yake ya kikazi ya kukagua utendaji kazi wa Mamlaka
ya Mapato Tanzania TRA.
Waziri
Kijaji amesema kuwa Wazabuni wameshalipwa kiasi cha shilingi bilioni 67.2,
Wakandarasi wamelipwa kiasi cha shilingi bilioni 24.2 na watoa huduma
mbalimbali wameshalipwa shilingi bilioni 38 na Watumishi wa umma bilioni 37 na Wadaiwa
wakilipwa bilioni 24.
Aidha, Dk.
Kijaji amesema kuwa hiyo ni dhamira njema iliyochukuliwa na serikali baada ya
kumaliza zoezi la uhakiki kwa kudhibiti malipo ya madeni hewa yasiostahili kwa
lengo la kufanikisha malipo hayo kwa wakandarasi waliotoa huduma kwa serikali
Kwa
upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Mkoa huo Bw. Seif
Mkude ameipongeza serikali kwa jitihada za kuhamasisha ulipaji kodi kwa manufaa
ya taifa kwa kuwa bila mapato nchi
haitaweza kuendelea.
SERIKALI IMELIPA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI MIA MOJA NA TISINI IKIWA NI MADENI YA WAKANDARASI NA WAZABUNI.
Reviewed by safina radio
on
October 18, 2017
Rating:

No comments