RAIS WA TANZANIA MH. JOHN MAGUFULI KUFUNGUA MKUTANO WA 33 WA JUMUIYA ZA SERIKALI ZA MITAA KESHO
TAREHE 02-10-201
![]() |
RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH. JOHN MAGUFULI |
Rais wa Jamuhuri
ya Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli kesho anatarajiwa kufungua mkutano wa
33 wa jumuiya za serikali za mitaa (ALAT)Jijini Dar-es-salaam.
Hayo yameelezwa
na meya wa jiji la Dar-es-salaam Mh Isaya Mwita wakati akizungumza na waandishi
wa habari jijini humo,ambapo amesema kuwa mkutano huo utawajumuisha wajumbe
mbalimbali kutoka mikoa yote ya Tanzania.
Amesema kuwa
mkutano huo utafungwa octoba 16 mwaka huu,ambapo pia wanatarajia kuwasilisha
maombi rasmi kwa rais Magufuli ya kurejesha vyanzo vya mapato vilivyochukuliwa
na serikali kuu viweze kurudishwa katika halmashauri ili ziweze kuongeza uwezo
wa kujiendesha.
Kwa upande wake
mmoja wa wajumbe wanaotarajia kuhudhuria mkutano huo Mh Haji Mnasi ambaye ni
mkurugenzi wa wilaya ya Songwe amesema ku katika mkutano huo wanatarajia
kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo namna ya kukabiliana na changamoto wanazokabiliana nazo katika maeneo yao ya kazi
pamoja na kubadilishana uzoefu.
RAIS WA TANZANIA MH. JOHN MAGUFULI KUFUNGUA MKUTANO WA 33 WA JUMUIYA ZA SERIKALI ZA MITAA KESHO
Reviewed by safina radio
on
October 02, 2017
Rating:

No comments