WATU WAWILI WAUAWA NCHINI UFARANSA KWA KUDUNGWA VISU

TAREHE 02-10-2017


Kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS limedai kufanya shambulizi la kudunga visu lililouwa watu wawili katika mji wa Kusini mwa Ufaransa wa Marseille, na kuwajeruhi wengine kadhaa.

Polisi wa kupambana na ugaidi wamesema wameanzisha uchunguzi kuhusu mashambulizi hayo, wakiyatazama kama mauaji yenye uhusiano na ugaidi, na jaribio la kuuwa maafisa wa serikali.


Kwa upande wake rais wa nchi hiyo Emmanuel Macron Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, amesema ameghadhibishwa na mashambulizi hayo.
WATU WAWILI WAUAWA NCHINI UFARANSA KWA KUDUNGWA VISU WATU    WAWILI  WAUAWA   NCHINI UFARANSA  KWA KUDUNGWA   VISU Reviewed by safina radio on October 02, 2017 Rating: 5

No comments