HALMASHAURI ZINAZODAIWA NA BODI YA MIKOPO ZATAKIWA KUREJESHA FEDHA HIZO
13-10-2017
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa-TAMISEMI Seleman Jaffo amemwagiza Mtendaji Mkuu wa Bodi ya
Mikopo ya Serikali za Mitaa Nchini kuhakikisha kuwa Halmashauri zinazodaiwa na
Bodi hiyo kwa muda mrefu zinarejesha fedha hizo ifikapo Desemba 30 mwaka huu.
Waziri Jaffo ametoa
agizo hilo baada ya kubaini kuwa Halmashauri kumi na mbili nchini hazijarejesha
mikopo ya zaidi ya shilingi bilioni mbili jambo ambalo limesababisha
halmashauri nyingine kushindwa kukopeshwa.
Aidha, Waziri Jaffo
amesema kuwa yeye amepewa dhamana ya kuiongoza ofisi hiyo, hivyo
hangependa wala kuridhika kwa utendaji
wa chombo hicho ambacho kipo chini ya wizara yake kulegalega.
Mbali na hayo, Waziri
Jaffo akamwagiza Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Mikopo hiyo ya serikali za mitaa
kwamba afuatilie wadaiwa wote sugu ambao wameshindwa kurejesha mikopo yao kama
ilivyoainishwa katika mikataba sahihi na iliyohalali ya urejeshaji wa
mikopo hiyo.
Kwa upande wake,
Mtendaji Mkuu wa Bodi hiyo Richard Mfugale amesema kuwa hadi kufikia Septemba
30 mwaka huu Bodi hiyo imekwisha toa mikopo yenye thamani ya zaidi ya Shilingi
Bilioni 9.7 za Kitanzania kwa Halmashauri hamsini na nne hapa nchini.
HALMASHAURI ZINAZODAIWA NA BODI YA MIKOPO ZATAKIWA KUREJESHA FEDHA HIZO
Reviewed by safina radio
on
October 13, 2017
Rating:

No comments