WATU ZAIDI YA 20 WAMEFARIKI KUTOKANA NA KIMBUNGA.
TAREHE 06-10-2017
Kimbunga kijulikanacho kama Nate
kimewaua watu zaidi ya 20 nchini Costa Rica, Nicaragua na Honduras huku
kikielekea kaskazini upande wa Marekani.
Hali ya dharura imetangazwa katika mataifa kadha ya Amerika ya Kati ambapo
watu zaidi ya 20 bado hawajulikani walipo,ambapo Kimbunga hicho kimesababisha
mvua kubwa, maporomoko ya ardhi na mafuriko.
Barabara nyingi hazipitiki, madaraja yameporomoka na pia kimesababisha
uharibifu mkubwa kwenye nyumba za watu na majengo.
Nchini Costa Rica, watu karibu laki nne hawana maji na maelfu wengine
wameachwa bila makao na wanalala kwenye vyumba vya muda na watu zaidi ya sita
wamethibitishwa kufariki katika taifa hilo.
Hata hivyo Watu watatu wameuawa nchini Honduras na kuna watu kadha ambao
hawajulikani waliko.
WATU ZAIDI YA 20 WAMEFARIKI KUTOKANA NA KIMBUNGA.
Reviewed by safina radio
on
October 06, 2017
Rating:

No comments