RAIA WA LIBERIA WAPIGA KURA KUMCHAGUA RAIS LEO

TAREHE 10-10-2017

Raia wa Liberia leo wanapiga kura kumchagua kiongozi mpya atakayemrithi Rais Ellen Johnson Sirleaf ambaye amekuwa madarakani kwa miaka 12.

Wapiga kura wana matumaini kuwa kiongozi mpya ataweza kuufufua uchumi wa taifa hilo, na kudumisha amani baada ya nchi hiyo kutumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kuanzia mwaka 1989 hadi 2003.

Wagombea 20 wanawania urais na miongoni mwao yupo mwanasoka maarufu wa zamani George Weah, makamu wa rais wa sasa Jospeh Boakai, kiongozi wa muda mrefu wa upinzani Charles Brumskine na mfanyabishara tajiri Alexander Cummings.


 Mwanamke pekee anayewania urais ni MacDella Cooper, ambaye ana ndoto za kufuata nyayo za Sirleaf ambaye ni mwanamke wa kwanza kuwa rais Afrika,ambapo vituo vya kupigia kura  vimefunguliwa  saa mbili asubuhi  na vitafungwa  saa kumi na mbili jioni, huku matokeo ya awali yakitarajiwa kutangazwa saa 48 baada ya uchaguzi.
RAIA WA LIBERIA WAPIGA KURA KUMCHAGUA RAIS LEO RAIA WA LIBERIA WAPIGA KURA KUMCHAGUA RAIS LEO Reviewed by safina radio on October 10, 2017 Rating: 5

No comments